Wednesday, 30 October 2019

SHAIRI KUHUSU MGOMO

                                      SHULE YA KINYAA
uongozi wenye haki, nimeishi kutamani,
lakini hausikiki, hata nikiwa makini,
ndo mana mi ni shabiki, wa waendao nyumbani,
shule yetu ya kinyaa, taa leo kawa moto,

unapowatamalaki, tajiri na maskini,
usiwaulize laki, walipe pasi na deni,
unawapa nne wiki, kuwatoa darasani,
shule yetu ya kinyaa, taa leo kawa moto,

hili haliaminiki, kutimu sasa faini,
ambayo hailipiki, kaongeza Firauni,
inafaa mshaliki, ndo turudi darasani,
shule yetu ya kinyaa, taa leo kawa moto,

usifosi halaiki, wapite njia fulani,
nafikiri wana haki, kupita barabarani,
usiwatie hamaki, kuwafosi jukwaani
shule yetu ya kinyaa, taa leo kawa moto,

huku kumejaa taki, takataka na sabuni,
eti mliwataliki, wafanyakazi kwa nini,
sasa tumesadiki, sisi hamtujalini,
shule yetu ya kinyaa, taa leo kawa moto,

kweli haiaminiki, ukuta wa nyayo chini,
karao wawe lukuki, sisi tuko milioni,
wakitumia bunduki, sisi mawe mikononi,
shule yetu ya kinyaa, taa leo kawa moto.

SHUKURANI
Mtunzi - Marc - Karash
0795936959SHAIRI KUHUSU MUGOMO


HADITHI YA KUSISIMUA

ANN NA MUTUVIE Jina lake ni Ann. Sura anayo ndio, umbo analo ndio pia tabasamu lake lingemvutia kila mtu kwenye gari waliyoisafiri. M...