Wednesday, 14 November 2018

HASIDI
Nasoma ushairini, Wa malenga Ben Njoka,
Kuhusu mtu fulani, hasidi atambulika,
Sifa yake ndiyo gani, tazama naimulika,
Wakati uko tabani, anakucheka moyoni,
Anakucheka moyoni, tatizo likikufika,
Huzuni anaubuni, pole akizitamka,
Na Kumbe ndani moyoni, hawezi koma kucheka,
Husuda humfitini, akikuona kileleni,
Akikuona kileleni, kwa wema ukisifika,
Atakesha msituni, waganga akiwasaka,
Wakuroge kwa makini, hadi upate kushuka,
Akiulizwa kwa nini, yeye kesi atabuni,
Yeye kesi atabuni, toto lake umebaka,
Akimbilie kotini, kufungua mashtaka,
Na ukishinda kesini, aseme ushikwe haka,
Anataka uwe duni, asikwone na fulani,
Asikwone na fulani, mkila ama kucheka,
Atamwendea jioni, rongo zake kuropoka,
Amsemee jamani, akili zimekuruka,
Usimpende fulani, atakurushia jini,
Atakurushia jini, akili itakuruka,
Akuseme kijijini, kono lako karefuka,
Pembe zote duniani, matope atakupaka,
Ben Njoka asemeni, hasidi sio shetani,
Hasidi sio shetani, nadhani yaeleweka,
Aweza kuwa jirani, ushindwe kumuepuka,
Una hasidi uani, wewe ishi kukumbuka,
Nasoma ushairini, wa malenga Ben Njoka,
Mtunzi -Marc karash
Kutoka-Embu
Kijiji -Kwandu -ambai
Simu. -0707090505/0795936965

HADITHI YA KUSISIMUA

ANN NA MUTUVIE Jina lake ni Ann. Sura anayo ndio, umbo analo ndio pia tabasamu lake lingemvutia kila mtu kwenye gari waliyoisafiri. M...